Wanasayansi waunda ubongo bandia Singapore

Jul 29, 2016, 04:47 AM

Wanasayansi wa Singapore wanadai kuwa wametengeneza ubongo bandia wa mwanadamu kwa mara ya kwanza. Wanasema kuwa ubongo huo mdogo utawapa nafasi bora zaidi ya kuelewa jinsi ya kuwasaidia wanaougua maradhi ya kutetemeka yajulikanayo katika Kiingereza kama Parkinson na pia kuchunguza zaidi dawa zinazotengenezwa kukabiliana na maradhi hayo.