Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametuma ujumbe wa rambirambi kwa Rais wa Zanzibar, Dkt Hussein kufuatia kifo cha Makamu wake wa Kwanza wa Rais Mhe. Seif Sharif Hamad.
Ikulu ya Kenya imeandika katika ukurasa wa twitter alikuwa kiongozi maarufu, mwenye busara na maendeleo na mchango wake kwa watu wake na ukanda wa Afrika Mashariki utakumbukwa.
Kiongozi wa chama cha CHADEMA, Tundu Lissu ametoa salamu za rambi rambi kufuatia kifo cha Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
Katika ukurasa wake wa Twitter Lissu amesema Maalim Seif alikuwa kiongozi mwenye ushawishi, na mtetezi wa Wazanzibari asiye na woga.
Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema Maalim Seif amekuwa nguzo muhimu ya ujenzi wa demokrasia ya vyama vingi katika taifa la Tanzania na mtetezi mkubwa wa maslahi ya Zanzibar.
Zitto ameyasema hayo wakati akitoa taarifa ya msiba wa Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha ACT-Wazalendo kwa Umma wa Watanzania.
''Ninajua kifo cha Maalim Seif kitawashtua na kuwafadhaisha wanachama wa ACT, Wazanzibari na Watanzania, ninapenda kuwahakikishia kuwa tutayaenzi maono yake aliyoyaishi wakati wa uhai wake''.
Amewataka Wazanzibari na Wanachama wa ACT-Wazalendo na Watanzania kwa ujumla wawe na utulivu katika kipindi hiki kigumu.
Meli ya kivita ya Marekani imekamata majahazi mawili yaliyobeba shehena haramu za silaha katika maji ya pwani ya Somalia, Jeshi la Wanamaji la Marekani limetangaza.
Silaha hizo zilikamatwa na meli aina ya USS Winston S Churchill wiki iliyopita wakati wa operesheni ya usalama, lakini tangazo hilo lilitolewa Jumanne.
Shehena ya silaha ilikuwa na maelfu ya bunduki za AK-47, bunduki nyepesi, bunduki nzito za aina ya sniper, vizindua vya roketi, Jeshi la Wanamaji la Marekani lilisema katika taarifa yake Shehena hiyo iligunduliwa wakati wa ukaguzi wa bendera, ingawa chanzo cha silaha hizo bado hakijatambuliwa.
"Kikosi hiki cha pamoja [jeshi, jeshi la wanamaji na walinzi wa pwani] kwenye meli ya Churchill walijumuika pamoja kufanikisha operesheni hii kwa muda wa siku mbili katika Bahari ya Hindi," Timothy Shanley, afisa mkuu wa Churchill, amenukuliwa akisema.
"Operesheni hizi huzuia shughuli za kusambaza misaada ya silaha kinyume cha sheria."
Rais Magufuli amuomboleza Maalim Seif Sharif Hamad
ACT-WazalendoCopyright: ACT-Wazalendo
Rais wa Tanzania, John Magufuli ameomboleza kifo cha Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Rais Magufuli ameeleza masikitiko yake kuhusu taarifa za kifo cha kiongozi huyo wa juu visiwa ni Zanzibar.
Akihutubia Taifa kwa njia ya televisheni, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hussein Mwinyi, alisema Maalim Seif alifariki dunia akiwa katika Taasisi ya Magonjwa ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa amelazwa kwa takribani wiki mbili.
''Majira ya saa tano na dakika 26 asubuhi Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad alifariki dunia, Maalim amefariki wakati akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Muhimbili ambapo alikuwa amelazwa tangu tarehe 9 mwezi Februari mwaka huu''. Alisema Rais Hussein Mwinyi.
Rais Mwinyi amesema taifa limepoteza kiongozi mzalendo na shupavu na ametangaza siku saba za maombolezo ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti.
Rais Mwinyi amesema taarifa zaidi kuhusu msiba na maziko yake zitaendelea kutolewa na serikali, kwa ushirikiano wa karibu na familia na Chama cha ACT- Wazalendo.
Nchi hiyo ilipokea chanjo ya AstraZeneca lakini ilisitisha kutolewa kwa chanjo hiyo baada ya kuwepo mashaka kuhusu ufanisi wake dhidi ya aina ya kirusi cha nchini humo.
Lakini wataalamu wa chanjo wa Shirika la Afya duniani wamesema hata nchi zenye aina ya virusi ambavyo kwanza vilibainika Afrika Kusini watumie chanjo ya AstraZeneca vaccine.
Kituo cha kupambana na kuzuia magonjwa Afrika(CDC) pia wamependekeza matumizi ya chanjo hiyo.
Mfanyabiashara wa Nigeria ahukumiwa Marekani kwa wizi wa mtandao
ForbesCopyright: Forbes
Mahakama ya Marekani imemhukumu kifungo cha miaka 10 gerezani mfanyabiashara kwa Kinigeria kwa kuendesha mtandao wa wizi wa mtandaoni na kuiba kiasi cha takribano pauni milioni 8.
Obinwanna Okeke, kwa jina jingine Invictus Obi, alitumia makampuni yenye makazi nchini Nigeria kuwadanganya watu katika jimbo la Virginia nchini Marekani.
Kampuni zake za 'Invictus Group companies' zilitumia barua pepe ili kupata taarifa za kuingia kwenye akaunti za watu kisha kuchukua fedha zao 2015 na mwaka 2019.
Obinwanna- ambaye aliwahi kuwa kwenye orodha ya forbes ya Wafanyabiashara wenye ushawishi wenye umri wa miaka 30- alikamatwa mwezi Agosti mwaka 2019.
Mahakama ya Rwanda kuanza kusikiliza kesi ya Paul Rusesabagina
Mahakama ya Rwanda hii leo inaanza kusikiliza kesi dhidi ya Paul Rusesabagina na
wengine 20 ambao wanakabiliwa na mashtaka ya ugaidi.
Rusesabagina,
mkosoaji wa Rais Paul Kagame, anatuhumiwa kuunga mkono shughuli za kikosi cha National Liberation (FLN), ambacho ni mrengo wa wanamgambo wa chama chake cha
Rwandan Movement for Democratic Change (MRCD).
Alikamatwa mnamo Agosti 2020 akiwa katika nchi ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kurudishwa nchini Rwanda kukabiliana na mashtaka ya ugaidi, utekaji nyara na mauaji.
Mwezi Julai mwaka 2018, FLN ilidai kuhusika na mashambulio katika mkoa wa kusini wa Rwanda.
BBCCopyright: BBC
Rusesabagina alifahamika kufuatia filamu ya Hotel Rwanda ikielezea jinsi alivyookoa maisha ya watutsi waliokuwa wamekimbilia katika hoteli moja mjini Kigali aliyokuwa meneja wake mwaka 1994.
Rais Paul Kagame amesema kikubwa sio ushujaa wa Bwana Rusesabagina au vitendo vyake wakati wa mauaji ya kimbari akisema kinachoangaliwa kwa sasa ni yeye.
Bwana Kagame amesema kwamba hajali kuhusu hadithi ya Bwana Rusesabagina kwamba yeye ni shujaa wa mauaji ya kimbari na kwamba ''hilo si jambo ambalo litakalomkabili mahakamani''.
"Kuna maswali ambayo lazima atayajibu.kuna wanaomsaidia wakiwa Ulaya,Marekani na kwingineko na ambao walimpandisha cheo na kumpa majina ya ushujaa.awe shujaa au la ,mimi sina wasi wasi na hilo.
Bobi Wine amtaka Jaji Mkuu kutosikiliza shauri lake
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Kiongozi wa upinzani Robert
Kyagulanyi maarufu Bobi Wine , amemtaka jaji Mkuu kujiondoa katika kusikiliza shauri la kupinga
kuchaguliwa tena Rais Yoweri Museveni.
Bobi Wine amemshutumu
jaji Alfonse Owiny- Dollo kwa upendeleo kwa sababu ya ushirika wake na rais.
Mwanasiasa wa upinzani
pia anataka majaji wengine wawili wa mahakama ya juu kujiondoa kusikiliza
shauri hilo kwa misingi hiyo hiyo.
Majaji watatu
hawajajibu chochote kuhusu shutuma dhidi yao.
Jaji Mkuu Owiny-Dollo
alikuwa mwanasheria wa Rais Museveni mwaka 2006, kwa mujibu wa tovuti ya Nile
Post.
Jaji Mike Chibita
alikuwa msaidizi wa Museveni katika masuala ya sheria, wakati Jaji Ezekiel
Muhanguzi ni ndugu wa Waziri wa Ulinzi Elly Tumwine kwa mujibu wa vyombo vya
habari vya nchini humo.
Bobi Wine amedai kuwa
watatu hao hawataweza kutenda haki iwapo watasikiliza shauri hilo.
Habari za moja kwa moja
Na Lizzy Masinga
time_stated_uk
Na kufukia hapo tunakamilisha matangazo haya mubashara.
Zitto Kabwe amuomboleza Maalim Seif
Tazama Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alivyomuomboleza Maalim Seif Sharif Hamad
Salamu za rambirambi zamiminika baada ya kifo cha Maalim Seif
Salamu za rambi rambi zimekuwa zikimiminika ndani na nje ya Tanzania baada ya kifo cha Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
Majira ya saa tano asubuhi Maalim seif aliaga dunia katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.
Viongozi mbalimbali wa ndani na nje na wanasiplomasia mbalimbali wameungana na Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla katika msiba huu.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Donald J. Wright amesema ni kiongozi aliwaweka watu wake mbele kwanza kabla ya madaraka.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametuma ujumbe wa rambirambi kwa Rais wa Zanzibar, Dkt Hussein kufuatia kifo cha Makamu wake wa Kwanza wa Rais Mhe. Seif Sharif Hamad.
Ikulu ya Kenya imeandika katika ukurasa wa twitter alikuwa kiongozi maarufu, mwenye busara na maendeleo na mchango wake kwa watu wake na ukanda wa Afrika Mashariki utakumbukwa.
Tundu Lissu: Maalim Seif alikuwa kiongozi shupavu
Kiongozi wa chama cha CHADEMA, Tundu Lissu ametoa salamu za rambi rambi kufuatia kifo cha Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
Katika ukurasa wake wa Twitter Lissu amesema Maalim Seif alikuwa kiongozi mwenye ushawishi, na mtetezi wa Wazanzibari asiye na woga.
Mfahamu Maalim Seif katika siasa za Tanzania?
Zitto Kabwe:Maalim Seif amekuwa nguzo muhimu
Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema Maalim Seif amekuwa nguzo muhimu ya ujenzi wa demokrasia ya vyama vingi katika taifa la Tanzania na mtetezi mkubwa wa maslahi ya Zanzibar.
Zitto ameyasema hayo wakati akitoa taarifa ya msiba wa Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha ACT-Wazalendo kwa Umma wa Watanzania.
''Ninajua kifo cha Maalim Seif kitawashtua na kuwafadhaisha wanachama wa ACT, Wazanzibari na Watanzania, ninapenda kuwahakikishia kuwa tutayaenzi maono yake aliyoyaishi wakati wa uhai wake''.
Amewataka Wazanzibari na Wanachama wa ACT-Wazalendo na Watanzania kwa ujumla wawe na utulivu katika kipindi hiki kigumu.
Unaweza pia kusoma
Shehena ya silaha haramu yakamatwa Somalia
Meli ya kivita ya Marekani imekamata majahazi mawili yaliyobeba shehena haramu za silaha katika maji ya pwani ya Somalia, Jeshi la Wanamaji la Marekani limetangaza.
Silaha hizo zilikamatwa na meli aina ya USS Winston S Churchill wiki iliyopita wakati wa operesheni ya usalama, lakini tangazo hilo lilitolewa Jumanne.
Shehena ya silaha ilikuwa na maelfu ya bunduki za AK-47, bunduki nyepesi, bunduki nzito za aina ya sniper, vizindua vya roketi, Jeshi la Wanamaji la Marekani lilisema katika taarifa yake Shehena hiyo iligunduliwa wakati wa ukaguzi wa bendera, ingawa chanzo cha silaha hizo bado hakijatambuliwa.
"Kikosi hiki cha pamoja [jeshi, jeshi la wanamaji na walinzi wa pwani] kwenye meli ya Churchill walijumuika pamoja kufanikisha operesheni hii kwa muda wa siku mbili katika Bahari ya Hindi," Timothy Shanley, afisa mkuu wa Churchill, amenukuliwa akisema.
"Operesheni hizi huzuia shughuli za kusambaza misaada ya silaha kinyume cha sheria."
Rais Magufuli amuomboleza Maalim Seif Sharif Hamad
Rais wa Tanzania, John Magufuli ameomboleza kifo cha Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Rais Magufuli ameeleza masikitiko yake kuhusu taarifa za kifo cha kiongozi huyo wa juu visiwa ni Zanzibar.
Akihutubia Taifa kwa njia ya televisheni, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hussein Mwinyi, alisema Maalim Seif alifariki dunia akiwa katika Taasisi ya Magonjwa ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa amelazwa kwa takribani wiki mbili.
''Majira ya saa tano na dakika 26 asubuhi Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad alifariki dunia, Maalim amefariki wakati akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Muhimbili ambapo alikuwa amelazwa tangu tarehe 9 mwezi Februari mwaka huu''. Alisema Rais Hussein Mwinyi.
Rais Mwinyi amesema taifa limepoteza kiongozi mzalendo na shupavu na ametangaza siku saba za maombolezo ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti.
Rais Mwinyi amesema taarifa zaidi kuhusu msiba na maziko yake zitaendelea kutolewa na serikali, kwa ushirikiano wa karibu na familia na Chama cha ACT- Wazalendo.
Pia unaweza kusoma
Afrika Kusini yapokea chanjo ya Johnson & Johnson
Afrika Kusini imepokea bechi ya kwanza ya chanjo ya Johnson & Johnson
Serikali imesema chanjo itahifadhiwa mahali salama katika jimbo la Gauteng na kisha kusambazwa kwenye majimbo mengine.
Chanjo hiyo itaanza kutolewa hivi karibuni.
Waziri wa Afya nchini humo, Zweli Mkhize alichapisha picha kwenye mtandao wa twitter kuwasili kwa bechi ya kwanza.
Nchi hiyo ilipokea chanjo ya AstraZeneca lakini ilisitisha kutolewa kwa chanjo hiyo baada ya kuwepo mashaka kuhusu ufanisi wake dhidi ya aina ya kirusi cha nchini humo.
Lakini wataalamu wa chanjo wa Shirika la Afya duniani wamesema hata nchi zenye aina ya virusi ambavyo kwanza vilibainika Afrika Kusini watumie chanjo ya AstraZeneca vaccine.
Kituo cha kupambana na kuzuia magonjwa Afrika(CDC) pia wamependekeza matumizi ya chanjo hiyo.
Mfanyabiashara wa Nigeria ahukumiwa Marekani kwa wizi wa mtandao
Mahakama ya Marekani imemhukumu kifungo cha miaka 10 gerezani mfanyabiashara kwa Kinigeria kwa kuendesha mtandao wa wizi wa mtandaoni na kuiba kiasi cha takribano pauni milioni 8.
Obinwanna Okeke, kwa jina jingine Invictus Obi, alitumia makampuni yenye makazi nchini Nigeria kuwadanganya watu katika jimbo la Virginia nchini Marekani.
Kampuni zake za 'Invictus Group companies' zilitumia barua pepe ili kupata taarifa za kuingia kwenye akaunti za watu kisha kuchukua fedha zao 2015 na mwaka 2019.
Obinwanna- ambaye aliwahi kuwa kwenye orodha ya forbes ya Wafanyabiashara wenye ushawishi wenye umri wa miaka 30- alikamatwa mwezi Agosti mwaka 2019.
Mahakama ya Rwanda kuanza kusikiliza kesi ya Paul Rusesabagina
Mahakama ya Rwanda hii leo inaanza kusikiliza kesi dhidi ya Paul Rusesabagina na wengine 20 ambao wanakabiliwa na mashtaka ya ugaidi.
Rusesabagina, mkosoaji wa Rais Paul Kagame, anatuhumiwa kuunga mkono shughuli za kikosi cha National Liberation (FLN), ambacho ni mrengo wa wanamgambo wa chama chake cha Rwandan Movement for Democratic Change (MRCD).
Alikamatwa mnamo Agosti 2020 akiwa katika nchi ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kurudishwa nchini Rwanda kukabiliana na mashtaka ya ugaidi, utekaji nyara na mauaji.
Mwezi Julai mwaka 2018, FLN ilidai kuhusika na mashambulio katika mkoa wa kusini wa Rwanda.
Rusesabagina alifahamika kufuatia filamu ya Hotel Rwanda ikielezea jinsi alivyookoa maisha ya watutsi waliokuwa wamekimbilia katika hoteli moja mjini Kigali aliyokuwa meneja wake mwaka 1994.
Rais Paul Kagame amesema kikubwa sio ushujaa wa Bwana Rusesabagina au vitendo vyake wakati wa mauaji ya kimbari akisema kinachoangaliwa kwa sasa ni yeye.
Bwana Kagame amesema kwamba hajali kuhusu hadithi ya Bwana Rusesabagina kwamba yeye ni shujaa wa mauaji ya kimbari na kwamba ''hilo si jambo ambalo litakalomkabili mahakamani''.
"Kuna maswali ambayo lazima atayajibu.kuna wanaomsaidia wakiwa Ulaya,Marekani na kwingineko na ambao walimpandisha cheo na kumpa majina ya ushujaa.awe shujaa au la ,mimi sina wasi wasi na hilo.
Bobi Wine amtaka Jaji Mkuu kutosikiliza shauri lake
Kiongozi wa upinzani Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine , amemtaka jaji Mkuu kujiondoa katika kusikiliza shauri la kupinga kuchaguliwa tena Rais Yoweri Museveni.
Bobi Wine amemshutumu jaji Alfonse Owiny- Dollo kwa upendeleo kwa sababu ya ushirika wake na rais.
Mwanasiasa wa upinzani pia anataka majaji wengine wawili wa mahakama ya juu kujiondoa kusikiliza shauri hilo kwa misingi hiyo hiyo.
Majaji watatu hawajajibu chochote kuhusu shutuma dhidi yao.
Jaji Mkuu Owiny-Dollo alikuwa mwanasheria wa Rais Museveni mwaka 2006, kwa mujibu wa tovuti ya Nile Post.
Jaji Mike Chibita alikuwa msaidizi wa Museveni katika masuala ya sheria, wakati Jaji Ezekiel Muhanguzi ni ndugu wa Waziri wa Ulinzi Elly Tumwine kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchini humo.
Bobi Wine amedai kuwa watatu hao hawataweza kutenda haki iwapo watasikiliza shauri hilo.
Habari! karibu katika matangazo ya moja kwa moja ya taarifa zetu