Got a TV Licence?

You need one to watch live TV on any channel or device, and BBC programmes on iPlayer. It’s the law.

Find out more
I don’t have a TV Licence.

Habari za moja kwa moja

Na Abdalla Seif Dzungu na Dinah Gahamanyi

time_stated_uk

  1. Rais Museveni atangaza maombalezo ya siku 14 Uganda kufuatia kifo cha Hayati Magufuli

    Museveni

    Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni amempongeza Samia Suluhu Hassan kwa kuwa Rais mpya wa Jamuhuru ya Muungano wa Tanzania baada ya kifo cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo Dkt John Pombe Magufuli.

    Katika taarifa iliyotumwa kwenye mtandao wake wa Twitter Bw Museveni amesema kuwa Uganda itafanya maombolezo ya siku 14 na kuongeza kuwa ''Roho yake ipumzike kwa amani''

    Ujumbe huo wa Rais Museveni pia umeambatanishwa na taarifa ya awali ya rambi rambi aliyoitoa Rais Museveni kwa familia ya Hayati Magufuli pamoja na Watanzania kwa ujumla, iliyomsifu Magufuli kama rafiki wa Uganda, na kiongozi thabiti aliyepigania maendeleeo ya Watanzania na wanaafrika kwa ujumla:

    View more on twitter
  2. Kwa picha: Viongozi wakuu wa Tanzania walivyouaga mwili wa Dkt John Pombe Magufuli

    Samia
    Image caption: Rais mpya wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akitoa heshima zake kwa mwili wa mtangulizi wake Hayati Dkt John Pombe magufuli
    Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa akiuaga mwili wa Hayati Dkt John Pombe Magufuli
    Image caption: Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa akitoa heshima zake kwa mwili wa Hayati Dkt John Pombe Magufuli
    Janeth Magufuli
    Image caption: Janeth Magufuli (katikati aliyevaa kitambaa), Mke wa Hayati Dkt John Pombe Magufuli akielekea kwenye jeneza lililokuwa na mwili wa mumewe, wakati Watanzania walipokuwa wakiuaga mwili huo katika uwanja wa taifa
  3. Kwa Picha: Umati wa watu ulifurika barabarani kuuaga mwili wa Dkt John Pombe Magufuli jijini Dar es Salaam

    Umati
    Image caption: Baadhi ya mitaa ya jiji la Dar es Salaam imefurika umati wa watu waliokuja kushuhudia msafara uliosafirisha mwili wa Hayati Dkt John Pombe Magufuli ili kumpa mkono wa buriani
    Umati
    Image caption: Badhi ya waombolezaji walikuwa na mabango yaliyoandikwa hisia zao kumuhusu Hayati Dkt John Pombe Magufuli
    Umati
    Image caption: Baadhi ya mitaa ya jiji la Dar es Salaam imefurika umati wa watu waliokuja kushuhudia msafara uliosafirisha mwili wa Hayati Dkt John Pombe Magufuli ili kumpa mkono wa buriani
    Umati
    Image caption: Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam walipanda juu ya miti na maeneo mengine ili walau kupata picha kwenye simu zao za mkononi za msafara ulioubeba mwili wa aliyekuwa rais wao, Hayati Dkt John Pombe Magufuli
  4. Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta atoa heshima zake kwa Hayati Dkt John Pombe Magufuli

    Uhuru

    Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta leo ametembelea ubalozi wa Tanzania nchini Kenya uliopo jijini Nairobi kutoa heshima zake kwa Hayati Dkt John Pombe Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 mwezi Machi.

    Rais Kenyatta alikuwa ameambatana na viongozi wakuu wakiwemo maspika wa mabunge mawili, Kaimu jaji wa Mahakama ya juu zaidi nchini humo, pamoja na mawaziri katika ubalozi huo kutoa heshima zake kwa Magufuli.

    Amesema “Tumekuja kuwahakikishia mshikamano nanyi katika wakati huu mgumu. Tunataka mfikishe rambi rambi zetu binafsi na zile za Wakenya kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

    “Tunamuombea. Tunataka mumhakikishie uunjaji mkono wetu na kwamba kazi nzuri ya kaka yetu (Rais Magufuli) imeanza, tutaendelea nayo ,”Rais Kenyatta alimwambia Balozi John Stephen Simbachawene ambaye alimpokea.

    Viongozi wa mabunge pia walitoa rambi rambi zao na kwa niaba ya mabunge waliyoyawakilisha.

    Ikulu ya rais mjini Nairobi imetoa taarifa hiyo kupitia mtandao wake wa Twitter:

    View more on twitter

    Katika taarifa yake kuhusu kifo cha aliyekuwa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, wiki hii Bw Kenyatta alisema amempoteza ''rafiki binafsi na kiongozi mwenzake''

  5. Kwa Picha: Hisia za majonzi na simanzi zatanda katika shughuli ya kuuaga mwili wa Rais Magufuli

    Majonzi
    Image caption: Umati wa wenye majonzi ya kumuaga aliyekuwa rais wao Dkt John Pombe Magufuli, ndani ya uwanja wa taifa jijini Dar es salaam
    Majonzi
    Majonzi
    Baadhi walionekana wafanya maombi binafsi  ya kuiombea roho ya Hayati Rais Dkt John Pombe Magufuli
    Image caption: Baadhi walionekana wakifanya maombi binafsi ya kuiombea roho ya Hayati Rais Dkt John Pombe Magufuli
    majonzi
    Majonzi
  6. Kwa picha: Hali ilivyo katika uwanja wa taifa Dar es Salaam katika shughuli ya kuuaga mwili wa Hayati Magufuli

    Hali
    Hali
    Hali
    Hali
    Hali
    Hali
    Hali
  7. Kwa picha: Mwili wa Hayati Dkt John Pombe Magufuli umeombewa katika kanisa la St.Peters

    Kanisani
    Image caption: Ibada ya wafu ikiendelea katika kanisa katoliki la St Peters jijini Dar es salaam kwa ajili ya Hayati Dkt John Pombe Magufuli

    Aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt John Pombe Magufuli, alikuwa muumini wa Kanisa Katoliki.

    Na mara kwa mara alionekana kanisani akihudhuria ibada katika siku za Jumapili.

    Kanisa la St Peters lililoko jijini Dar es Salaam ni moja ya makanisa ambapo alikuwa akienda kusali.

    Na leo Kanisa hilo limeupokea mwili wake na kuuombea katika ibada ya wafu.

    Waumini katika kanisa la kikatoliki la St.Peters jijini Dar es Salaam wakihudhuria Ibada ya kumuombea aliyekuwa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
    Image caption: Waumini katika kanisa la kikatoliki la St.Peters jijini Dar es Salaam wakihudhuria Ibada ya wafu ya kumuombea aliyekuwa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
  8. Mwili wa rais Magufuli ukiingizwa Kanisani Dar es Salaam

    Video content

    Video caption: Kifo cha Rais Magufuli: Mwili wa kiongozi huyo wawasili katika kanisa Dar es Salaam kwa ib
  9. Ibada ya kuuombea mwili wa Magufuli yaendelea

    baadhi waumini wakiingia katika kanisa la St Peters kuuaga mwili wa Magufuli
    Image caption: baadhi waumini wakiingia katika kanisa la St Peters kuuaga mwili wa Magufuli
    Wengine walishindwa kujizuia walipoona jeneza la Magufuli
    Image caption: Wengine walishindwa kujizuia walipoona jeneza la Magufuli
    Mke wa aliyekuwa rais wa Tanzania John Pombe Magufuli
    Image caption: Mke wa aliyekuwa rais wa Tanzania John Pombe Magufuli
    MMoja wa waombolezaji
    Image caption: Mmoja wa waombolezaji
    Baadhi ya waombolezaji wamevaa barakoa
    Image caption: Baadhi ya waombolezaji wamevaa barakoa
    Vikosi vya usalama vikiusindikiza mwili wa Hayati Dkt John Pombe Magufuli
    Image caption: Vikosi vya usalama vikiusindikiza mwili wa aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt John Pombe Magufuli
    Baadhi ya waombolezaji wakiuza  baji za picha ya Hayati Magufuli mjini Dar es Salaam
    Image caption: Baadhi ya waombolezaji wakiuza baji za picha ya Hayati Magufuli mjini Dar es Salaam
    Umati wa waombolezaji  katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam
    Image caption: Umati wa waombolezaji katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam
  10. Mwili wa Magufuli waagwa Dar es Salaam

    Ibada ya kuuombea na kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania John Pombe Magufuli inaendelea katika kanisa la St Peters Jiji Dar es Salaam.

  11. Natumai hamjambo. Ni siku nyengine ambapo tutawaangazieni mubashara matangazo ya kifo cha rais John Pombe Magufuli