Rais Museveni atangaza maombalezo ya siku 14 Uganda kufuatia kifo cha Hayati Magufuli
ReutersCopyright: Reuters
Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni amempongeza Samia Suluhu Hassan kwa kuwa Rais mpya wa Jamuhuru ya Muungano wa Tanzania baada ya kifo cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo Dkt John Pombe Magufuli.
Katika taarifa iliyotumwa kwenye mtandao wake wa Twitter Bw Museveni amesema kuwa Uganda itafanya maombolezo ya siku 14 na kuongeza kuwa ''Roho yake ipumzike kwa amani''
Ujumbe huo wa Rais Museveni pia umeambatanishwa na taarifa ya awali ya rambi rambi aliyoitoa Rais Museveni kwa familia ya Hayati Magufuli pamoja na Watanzania kwa ujumla, iliyomsifu Magufuli kama rafiki wa Uganda, na kiongozi thabiti aliyepigania maendeleeo ya Watanzania na wanaafrika kwa ujumla:
Kwa picha: Viongozi wakuu wa Tanzania walivyouaga mwili wa Dkt John Pombe Magufuli
Kwa Picha: Umati wa watu ulifurika barabarani kuuaga mwili wa Dkt John Pombe Magufuli jijini Dar es Salaam
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta atoa heshima zake kwa Hayati Dkt John Pombe Magufuli
State House /TwitterCopyright: State House /Twitter
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta leo ametembelea ubalozi wa Tanzania nchini Kenya uliopo jijini Nairobi kutoa heshima zake kwa Hayati Dkt John Pombe Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 mwezi Machi.
Rais Kenyatta alikuwa
ameambatana na viongozi wakuu wakiwemo maspika wa mabunge mawili, Kaimu
jaji wa Mahakama ya juu zaidi nchini humo, pamoja na mawaziri katika ubalozi huo kutoa heshima zake kwa Magufuli.
Amesema “Tumekuja kuwahakikishia mshikamano nanyi katika
wakati huu mgumu. Tunataka mfikishe rambi rambi zetu binafsi na zile za Wakenya kwa
Rais Samia Suluhu Hassan.
“Tunamuombea. Tunataka mumhakikishie uunjaji mkono wetu na
kwamba kazi nzuri ya kaka yetu (Rais Magufuli) imeanza, tutaendelea nayo ,”Rais Kenyatta
alimwambia Balozi John Stephen Simbachawene ambaye
alimpokea.
Viongozi wa mabunge pia
walitoa rambi rambi zao na kwa niaba ya mabunge waliyoyawakilisha.
Ikulu ya rais mjini Nairobi imetoa taarifa hiyo kupitia mtandao wake wa Twitter:
Katika taarifa yake kuhusu kifo cha aliyekuwa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, wiki hii Bw Kenyatta alisema amempoteza ''rafiki binafsi na kiongozi mwenzake''
Kwa Picha: Hisia za majonzi na simanzi zatanda katika shughuli ya kuuaga mwili wa Rais Magufuli
BBCCopyright: BBC
BBCCopyright: BBC
BBCCopyright: BBC
BBCCopyright: BBC
Kwa picha: Hali ilivyo katika uwanja wa taifa Dar es Salaam katika shughuli ya kuuaga mwili wa Hayati Magufuli
BBCCopyright: BBC
BBCCopyright: BBC
BBCCopyright: BBC
BBCCopyright: BBC
BBCCopyright: BBC
BBCCopyright: BBC
BBCCopyright: BBC
Kwa picha: Mwili wa Hayati Dkt John Pombe Magufuli umeombewa katika kanisa la St.Peters
Aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt John Pombe Magufuli, alikuwa muumini wa Kanisa Katoliki.
Na mara kwa mara alionekana kanisani akihudhuria ibada katika siku za Jumapili.
Kanisa la St Peters lililoko jijini Dar es Salaam ni moja ya makanisa ambapo alikuwa akienda kusali.
Na leo Kanisa hilo limeupokea mwili wake na kuuombea katika ibada ya wafu.
Mwili wa rais Magufuli ukiingizwa Kanisani Dar es Salaam
Ibada ya kuuombea mwili wa Magufuli yaendelea
Mwili wa Magufuli waagwa Dar es Salaam
Ibada ya kuuombea na kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania John Pombe Magufuli inaendelea katika kanisa la St Peters Jiji Dar es Salaam.
Natumai hamjambo. Ni siku nyengine ambapo tutawaangazieni mubashara matangazo ya kifo cha rais John Pombe Magufuli
Habari za moja kwa moja
Na Abdalla Seif Dzungu na Dinah Gahamanyi
time_stated_uk
Rais Museveni atangaza maombalezo ya siku 14 Uganda kufuatia kifo cha Hayati Magufuli
Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni amempongeza Samia Suluhu Hassan kwa kuwa Rais mpya wa Jamuhuru ya Muungano wa Tanzania baada ya kifo cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo Dkt John Pombe Magufuli.
Katika taarifa iliyotumwa kwenye mtandao wake wa Twitter Bw Museveni amesema kuwa Uganda itafanya maombolezo ya siku 14 na kuongeza kuwa ''Roho yake ipumzike kwa amani''
Ujumbe huo wa Rais Museveni pia umeambatanishwa na taarifa ya awali ya rambi rambi aliyoitoa Rais Museveni kwa familia ya Hayati Magufuli pamoja na Watanzania kwa ujumla, iliyomsifu Magufuli kama rafiki wa Uganda, na kiongozi thabiti aliyepigania maendeleeo ya Watanzania na wanaafrika kwa ujumla:
Kwa picha: Viongozi wakuu wa Tanzania walivyouaga mwili wa Dkt John Pombe Magufuli
Kwa Picha: Umati wa watu ulifurika barabarani kuuaga mwili wa Dkt John Pombe Magufuli jijini Dar es Salaam
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta atoa heshima zake kwa Hayati Dkt John Pombe Magufuli
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta leo ametembelea ubalozi wa Tanzania nchini Kenya uliopo jijini Nairobi kutoa heshima zake kwa Hayati Dkt John Pombe Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 mwezi Machi.
Rais Kenyatta alikuwa ameambatana na viongozi wakuu wakiwemo maspika wa mabunge mawili, Kaimu jaji wa Mahakama ya juu zaidi nchini humo, pamoja na mawaziri katika ubalozi huo kutoa heshima zake kwa Magufuli.
Amesema “Tumekuja kuwahakikishia mshikamano nanyi katika wakati huu mgumu. Tunataka mfikishe rambi rambi zetu binafsi na zile za Wakenya kwa Rais Samia Suluhu Hassan.
“Tunamuombea. Tunataka mumhakikishie uunjaji mkono wetu na kwamba kazi nzuri ya kaka yetu (Rais Magufuli) imeanza, tutaendelea nayo ,”Rais Kenyatta alimwambia Balozi John Stephen Simbachawene ambaye alimpokea.
Viongozi wa mabunge pia walitoa rambi rambi zao na kwa niaba ya mabunge waliyoyawakilisha.
Ikulu ya rais mjini Nairobi imetoa taarifa hiyo kupitia mtandao wake wa Twitter:
Katika taarifa yake kuhusu kifo cha aliyekuwa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, wiki hii Bw Kenyatta alisema amempoteza ''rafiki binafsi na kiongozi mwenzake''
Kwa Picha: Hisia za majonzi na simanzi zatanda katika shughuli ya kuuaga mwili wa Rais Magufuli
Kwa picha: Hali ilivyo katika uwanja wa taifa Dar es Salaam katika shughuli ya kuuaga mwili wa Hayati Magufuli
Kwa picha: Mwili wa Hayati Dkt John Pombe Magufuli umeombewa katika kanisa la St.Peters
Aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt John Pombe Magufuli, alikuwa muumini wa Kanisa Katoliki.
Na mara kwa mara alionekana kanisani akihudhuria ibada katika siku za Jumapili.
Kanisa la St Peters lililoko jijini Dar es Salaam ni moja ya makanisa ambapo alikuwa akienda kusali.
Na leo Kanisa hilo limeupokea mwili wake na kuuombea katika ibada ya wafu.
Mwili wa rais Magufuli ukiingizwa Kanisani Dar es Salaam
Ibada ya kuuombea mwili wa Magufuli yaendelea
Mwili wa Magufuli waagwa Dar es Salaam
Ibada ya kuuombea na kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania John Pombe Magufuli inaendelea katika kanisa la St Peters Jiji Dar es Salaam.
Natumai hamjambo. Ni siku nyengine ambapo tutawaangazieni mubashara matangazo ya kifo cha rais John Pombe Magufuli