Kifo cha Rais Magufuli: Wasanii wa muziki Tanzania wamlilia Magufuli

Kifo cha Rais Magufuli: Wasanii wa muziki Tanzania wamlilia Magufuli

Baadhi ya Wasanii wa muziki nchini Tanzania wamekuwa wakielezea hisia zao za huzuni kuhusu kifo cha rais wa nchi hiyo Dkt John Pombe Magufuli ambaye amefariki dunia jana kutokana na maradhi ya moyo.

Wasanii hao ambao ni pamoja na Diamond Platnumz, RayVanny, Jux, Marioo, Malkia Karen, Zuchu, Khadija Kopa, Christina Shusho, wamejikusanya na kuingia studio kuandaa wimbo wa pamoja wa kumuaga Rais Dkt. John Pombe Magufuli