Cyprian Kizito Lwanga: Askofu mkuu wa Kanisa Katoliki Kampala amefariki

  • Issac Mumena
  • BBC Swahili Kampala
Viongozi wa kidini wanataka uchaguzi mkuu uahirishwe kwa miaka mitatu

Chanzo cha picha, TWITTER

Maelezo ya picha, Rais Museveni na Askofu Mkuu wa Kampala Cyprian Lwanga Kizito

Askofu mkuu wa Kanisa Katoliki mjini Kampala Cyprian Kizito Lwanga amefariki akiwa na umri wa miaka 68, Kanisa limethibitisha

Katika taarifa iliyotolewa na Diyosisi ya Kampala ya Kanisa Katoliki, Askofu Lwanga alipatikana chumbani mwake akiwa amefariki Jumamosi asubuhi. Chanzo cha kifo chake hakijabainishwa.

Taarifa za kifo hicho cha ghafla zimewashtua Waganda wengi ambao wametumia twitter na WhatsApp kutoa rambirambi zao.

Mapema Ijumaa, aliongoza Wakristo katika ibaada ya Ijumaa njema akishirikiana na Askofu mkuu wa kanisa la Uganda Daktari Kazimba Mugalu,kupitia Baraza la Muungano wa Madhehebu ya Wakristo nchini Uganda (UJCC), ambalo alikuwa mwenyekiti wake.

Kizito Lwanga aliyetawazwa kuwa padri wa Kanisa Katolikio 1978 alionekana kama mkosoaji wa serikali ya NRM.

ALikuwa akiangazia wazi wazi dhidi ya ufisadi, ukiukaji wa haki za binadamu na marekebisho ya katiba ya nchi ili kuondoa ukomo wa muhula na urais ili kumruhusu Rais aliye madarakani, Yoweri Museveni kuongeza muda wa utawala wake.

Mwaka 2012 aliwahi kumuandikia barua Rais Museveni akimtaka astaafu ifikapo mwaka 2016.

Kifo chake kimepokelewaje?

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine aliandika katika mtandao wa Twitter: Nimepokea kwa mshtuko kifo cha ghafla cha Dkt. Cyprian Kizito Lwanga, Askofu Mkuu wa Kampala. Itakuwa vigumu kukabiliana na msiba huu.

Ruka Twitter ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Mwisho wa Twitter ujumbe, 1

Mwaka 2018, Askofu huyo mkuu aliilaumu utawala wa Museveni kwa kuwatumia makasisi kumchunguza alipokuwa akipinga madai kwamba anapanga kupindua serikali.

Hivi karibuni, alilaani visa vya kukamatwa na kutekwa nyara kwa wafuasi wa upinzani.

Wakati wa uchaguzi wa mwezi Januari January 2021, alipendekeza uchaguzi kuahirishwa kwa kipindi cha miaka mitatu kutokana na janga la corona na kupanda kwa taharuki za kisiasa.

Mrengo wa upinzani ulipiga pendekezo hilo.

Katika Ibaada ya jana alimpongeza aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati John Pombe Magufuli kwa kazi alizowafanyia Watanzania na Jumuia ya Afrika mashariki kwa muda mfupi katika utawala wake.

Pia alisifu utawala uliopo kwa kuingia madarakani wakati huo mgumu baada ya kifo cha John Pombe Magufuli na kusema liwe funzo kwa mataifa mengine.

Askofu mkuu wa Kampala Cyprian Kizito

Chanzo cha picha, Mitandao ya Kijamii

Katika ujumbe wake wa Ijumaa kuu hapo pia aliomba serikali kuwaachia huru waliowatekwa nyara au kukamatwa bila kufikishwa mbele ya sheria.

Askofu Lwanga alizaliwa mwaka 1953 wilayani Mukono mashariki ya mji wa Kampala.

Kifo cha Lwanga kimetokea wakati Uganda inakabiliwa na mgawanyiko mkubwa wa kisiasa kufuatia uchaguzi uliokuwa na ushindani mkali huku upinzani ukidai kuwa baadhi ya wafuasi wao wametekwa.