Got a TV Licence?

You need one to watch live TV on any channel or device, and BBC programmes on iPlayer. It’s the law.

Find out more
I don’t have a TV Licence.

Habari za moja kwa moja

Na Asha Juma

time_stated_uk

  1. Na kufikia hapo ndio tunakamilisha matangazo yetu kwa leo. Kwaheri.

  2. Iran italipa kwa wakati unaofaa kwetu - waziri wa Israeli

    .

    Israel "itajibu" mashambulizi ya Iran dhidi ya nchi hiyo wakati ufaao, waziri wa masuala ya vita Benny Gantz anasema.

    Katika taarifa iliyotolewa muda mfupi uliopita - kabla tu ya baraza la mawaziri linaloangazia masuala ya vita nchini Israel kuitishwa - Gantz anasema: "Tutaunda muungano wa kikanda na Iran itagharamika kwa mtindo na wakati unaofaa kwetu.

    "Na muhimu zaidi, tukikabiliwa na hamu ya maadui zetu kutudhuru, tutaendelea kuungana na kuwa na nguvu imara."

    Gantz anasema amemaliza kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Annalena Baerbock.

    "Tulijadili kwanza kabisa umuhimu wa kuunda umoja wa kimataifa ili kukabiliana na uchokozi wa Iran moja kwa moja na kupitia washirika wake - kikanda na kimataifa," Gantz anasema katika ujumbe wa kwenye mtandao wa kijamii.

    Baraza la mawaziri la vita la Israel lilianza kukutana saa 15:00 kwa saa za eneo.

  3. Macho yote sasa yanatazama jinsi Israel itakavyojibu shambulizi la Iran

    .

    Jeshi la Israel linasema asilimia 99 ya makombora na ndege zisizo na rubani zilizorushwa na Iran usiku kucha zilinaswa bila kulenga shabaha zao.

    Iran ilisema shambulio hilo lilitokana na shambulio baya dhidi ya makao ya wanadiplomasia wa Iran nchini Syria wiki mbili zilizopita.

    Kipi kinafuata kutokea hapa inategemea kwa kiasi kikubwa jinsi Israel itakavyoamua namna ya kujibu mashambulizi ya jana usiku.

    Nchi za eneo hilo na kwingineko, zikiwemo zile ambazo hazipendi sana utawala wa Iran, zimehimiza kujizuia.

    Msimamo wa Iran ni pamoja na: "Sasa mambo yako sawa, huo ndio mwisho wa jambo hilo, usitushambulie tena la sivyo tutapanga mashambulizi mabaya zaidi dhidi yako ambayo hutaweza kuzuia."

    Lakini, Israel tayari imeapa kuchukua hatua ya "kujibu" na serikali yake mara nyingi imekuwa ikitajwa kuwa moja ya wenye msimamo mkali zaidi katika historia ya Israel.

    Soma zaidi:

    Iran yaonya kufanya shambulizi baya zaidi ikiwa Israel italipiza kisasi

    Israel yasema makabiliano ya Iran 'bado hayajaisha' baada ya kutungua ndege zisizo na rubani kutoka Tehran

  4. Israel na Marekani walikuwa wamejiandaa kwa mashambulizi ya Iran

    .

    Israel, kwa usaidizi wa Marekani, ilikuwa imejiandaa vyema kwa shambulizi la Iran.

    Taarifa ilikuwa imetumwa kwa telegraph mapema.

    Lakini jambo muhimu zaidi, Israel na Marekani walikuwa na mifumo ya kisasa ya ulinzi wa anga tayari.

    Israel imekuwa na uzoefu mwingi wa kutungua roketi kwa wakati mmoja na Hamas kutoka Gaza kwa miaka mingi.

    Israel ina ulinzi wa hali ya juu wa anga, ikiwa ni pamoja na mfumo wake wa Iron Dome, mfumo wa ulinzi wa anga wa David's Sling na Arrow - ambao umetumika kufyatua roketi za Hamas.

    Marekani pia imekuwa ikikabiliana na vitisho kama hivyo katika Bahari ya shamu kutungua ndege zisizo na rubani, makombora ya baharini na makombora ya balistiki yaliyorushwa na Wahouthi wanaoungwa mkono na Iran nchini Yemen.

    Ndege za Marekani kwenye meli ya USS Dwight D Eisenhower pia zimehusika katika kuharibu ndege zisizo na rubani za Houthi kutoka angani.

    Kwa maneno mengine, Israeli na Marekani tayari walijua walikuwa na uwezo wa kijeshi wa kufanikiwa kuzuia silaha za Iran.

    Soma zaidi:

    Zaidi ya ndege 300 zisizo na rubani na makombora zilirushwa dhidi ya Israel - IDF

    Marekani 'haitashiriki katika hatua zozote za kulipiza kisasi Iran', CNN inaripoti

  5. Zaidi ya ndege 300 zisizo na rubani na makombora zilirushwa dhidi ya Israel - IDF

    .

    Zaidi ya ndege 300 zisizo na rubani na makombora kutoka Iran, Iraq na Yemen zilirushwa dhidi ya Israel, msemaji wa jeshi la Israel amesema.

    Lt Kanali Peter Lerner ameiambia BBC Radio: "Ninajua kwamba karibu silaha 360 mbalimbali, droni 170 za vilipuzi, makombora 30 ya baharini, makombora 120 ya balestiki yalirushwa kuelekea Israel.

    "Mengine mengi yalizuiliwa". Aidha, BBC haiwezi kuthibitisha takwimu hizo kwa kujitegemea.

    Lerner anasema makombora ya cruise na UAVs "yalizuiwa kabla ya kufika kwenye anga la Israel".

    Ameongeza kuwa ulinzi wa anga la Israel na washirika wake kutoka Marekani, Uingereza, Ufaransa na mataifa mengine yalituma "ujumbe mkali sana" kwa Iran.

    Soma zaidi:

    Ufaransa ilisaidia kutulinda dhidi ya shambulio la Iran, linasema jeshi la Israel

    Marekani 'haitashiriki katika hatua zozote za kulipiza kisasi Iran', CNN inaripoti

    Israel: Hamas yakataa makubaliano ya hivi karibuni ya kusitisha mapigano

  6. Ufaransa ilisaidia kutulinda dhidi ya shambulio la Iran, linasema jeshi la Israel

    Jeshi la Israel linasema kuwa Ufaransa ilikuwa miongoni mwa nchi zilizohusika katika kuwalinda dhidi ya shambulio lililotokea usiku la Iran dhidi ya Israel.

    "Ufaransa ina teknolojia nzuri sana, ndege, rada na najua walikuwa wakichangia katika doria ya anga," msemaji mkuu wa jeshi la Israel amesema.

    Ameongeza kuwa hana maelezo kamili kama ndege za Ufaransa ziliangusha kombora lolote la Iran.

    Na kama tulivyotaja hapo awali, Uingereza, Marekani na Jordan pia zilisaidia katika juhudi hizo.

    Soma zaidi:

    Marekani 'haitashiriki katika hatua zozote za kulipiza kisasi Iran', CNN inaripoti

    Israel: Hamas yakataa makubaliano ya hivi karibuni ya kusitisha mapigano

  7. Marekani 'haitashiriki katika hatua zozote za kulipiza kisasi Iran', CNN inaripoti

    us

    Wachambuzi wanadhani kuwa shambulio hili ambalo halijawahi kushuhudiwa kutoka jimbo la Iran hadi katika eneo la Israel litasababisha hatua ya kulipiza kisasi na Israel.

    Hata hivyo, kwa mujibu wa CNN, ikimnukuu afisa wa utawala, Rais Joe Biden tayari amemwambia Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwamba Marekani haitashiriki katika operesheni yoyote ya mashambulizi dhidi ya Iran.

    Wakati huo huo, afisa wa Israel ameliambia gazeti la New York Times kwamba hatua yoyote ya kujibu shambulizi hilo itakayochukuliwa na Israel "itaratibiwa na washirika wake".

    Kama tulivyoripoti awali, Biden amesema kuwa Marekani iliisaidia Israel kuangusha karibu ndege zote zisizo na rubani 300 na makombora ambayo yalirushwa na Iran.

    Soma zaidi:

    Israel yadungua ndege 300 za Iran zisizo na rubani na makombora kwa usaidizi wa Marekani - IDF

    Biden ashutumu 'shambulio la Iran' na kuunga mkono usalama wa Israel

  8. Israel: Hamas yakataa makubaliano ya hivi karibuni ya kusitisha mapigano

    .

    Taarifa kuhusu mazungumzo ya kujaribu kupata mabadilishano ya mateka na wafungwa na kusitisha mapigano huko Gaza, zasema kuwa Hamas imekataa mpango wa hivi karibuni uliotolewa na wapatanishi, kwa mujibu wa shirika la kiintelijensia la Israel Mossad.

    Shirika la Israel linasema katika taarifa kuwa kukataliwa kwa wazo hilo "inathibitisha kwamba kiongozi wa Hamas huko Gaza Yahya Sinwar hataki kufikiwa kwa makubaliano ya kutolewa kwa misaada ya kibinadamu na kurejesha mateka".

    Hamas "inaendelea kuchochea mvutano wa Iran na inajitahidi kuhakikisha kuongezeka kwa mzozo huo katika kanda," taarifa hiyo inaendelea."

    Israel itaendelea kujitahidi kufikia malengo ya vita na Hamas kwa nguvu zote, na kuhakikisha mateka 133 wamerudishwa kutoka Gaza.

    Soma zaidi:

  9. 'Iran haitaki mambo kuwa mabaya zaidi'

    Dk Lina Khatib, mshirika mwenza katika Chatham House, ameiambia BBC Radio 5 Live kwamba shambulio la Iran "lilikusudiwa kuwa aina ya tukio ambalo Iran ilitaka ulimwengu ushuhudie".

    Dk Khatib, ambaye kwa sasa yuko nchini Lebanon, amesema "limeandaliwa sana" na "kwa kweli ni dogo".

    Alirejelea Iran ikitoa taarifa kwamba ilizingatia kulipiza kisasi kabla ya ndege zisizo na rubani kufikia maeneo yao lengwa nchini Israeli.

    "Kwa hivyo hii inaonyesha kwamba Iran ilitaka tu kutuma ujumbe mkali sana, ili ionekane kama imejibu moja kwa moja kwa Israel, lakini wakati huo huo haitaki suala hilo kuendelea zaidi."

    Soma zaidi:

  10. Israel yasema makabiliano ya Iran 'bado hayajaisha'

    .

    Kumekuwa na matukio kadhaa muhimu katika hatua ya Iran kuishambulia Israel moja kwa moja. Baadhi tu ya yaliyotokea kufikia sasa:

    • Jeshi la Israel lasema asilimia 99 ya msururu wa makombora na ndege zisizo na rubani zilizorushwa na Iran usiku kucha zilinaswa bila kulenga shabaha zao.
    • Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant amesema "uharibifu mdogo sana" umesababishwa kutokana na shambulio hilo - lakini akaongeza "kampeni bado haijaisha", akisema nchi lazima "ibaki macho" na kujiandaa kwa lolote linaloweza kutokea.
    • Waziri mkuu wa Israel amesema kwenye mitandao ya kijamii "tutashinda" , huku rais wa nchi hiyo Isaac Herzog akiyasifu majeshi ya nchi yake na kusema kuwa "wema utashinda nguvu za uovu"
    • Hili lilikuwa shambulio la kwanza la moja kwa moja la Iran dhidi ya Israel , likihusisha zaidi ya ndege zisizo na rubani 300 na makombora.
    • Iran inasema shambulio hilo "limefanikisha malengo yake yote" na lilikuwa ni kujibu shambulizi lililoua makamanda wa Iran huko Damascus tarehe 1 Aprili.
    • Siku ya Jumapili, Iran ilikariri onyo lake dhidi ya kulipiza kisasi, ikisema kuwa hii itasababisha hatua mbaya zaidi
    • Wakati huo huo, Marekani inaitisha mkutano wa viongozi wa G7 ili kuratibu namna watakavyojibu shambulio hilo

    Soma zaidi:

    Ulimwengu hauwezi kumudu vita vingine - UN

  11. Biden ashutumu 'shambulio la Iran' na kuunga mkono usalama wa Israeli

    Rais wa Marekani Joe Biden amewasifu wanajeshi wa Marekani ambao alisema "waliisaidia Israel kuangusha takriban ndege zote" zisizo na rubani na makombora yaliyorushwa na Iran siku ya Jumapili.

    Katika taarifa yake, alisema Marekani ilihamisha ndege na meli za kivita katika eneo hilo kabla ya shambulio ambalo halijawahi kutokea hapo kabla.

    "Ninalaani mashambulizi haya kwa nguvu zote," aliongeza.

    Israel ilisema Iran ilirusha makumi ya ndege zisizo na rubani na makombora kuelekea upande wake, ikiwa ni mara ya kwanza kuishambulia Israel moja kwa moja kutoka katika ardhi yake.

    Alisema "nyingi" zilinaswa, lakini kulikuwa na idadi ndogo ya ndege zilizoshambulia ikiwemo katika kambi ya IDF kusini mwa Israel. Takriban mtu mmoja, aliyeripotiwa kuwa msichana mdogo, alijeruhiwa.

    Iran hapo awali ilionya kuwa Israel "itaadhibiwa" kwa kushambulia ubalozi mdogo nchini Syria tarehe 1 Aprili, ambao uliua maafisa saba wa Iran akiwemo kamanda mkuu. Israel haijathibitisha au kukanusha ikiwa ilihusika na shambulizi hilo.

    "Nimezungumza na Waziri Mkuu [Benjamin] Netanyahu ili kuthibitisha kujitolea kwa Marekani kwa usalama wa Israel," Bw Biden alisema muda mfupi baada ya wawili hao kuzungumza kwa simu.

    "Nilimwambia kuwa Israel ilionyesha uwezo wa ajabu wa kujilinda na kushinda hata mashambulizi ambayo hayajawahi kushuhudiwa," aliongeza.

    Soma zaidi:

  12. Ulimwengu hauwezi kumudu vita vingine - UN

    ,

    Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani shambulizi la Iran dhidi ya Israel, akisema kwamba anazitaka pande zote kujizuia zaidi.

    "Ninaziomba pande zote kujizuia kwa kiwango cha juu ili kuepuka hatua yoyote ambayo inaweza kusababisha makabiliano makubwa ya kijeshi katika eneo jingine la Mashariki ya Kati," amesema katika taarifa yake.

    "Nimesisitiza mara kwa mara kwamba si kanda wala ulimwengu unaoweza kumudu vita vingine."

    Soma zaidi:

  13. Iran yaonya kufanya shambulizi baya zaidi ikiwa Israel italipiza kisasi

    .

    Iran imerejelea onyo kwa Israel siku ya Jumapili, ikisema haipaswi kujibu mashambulizi yake ambayo hayajawahi kushuhudiwa dhidi ya Israel na kwamba hatua zake zinazofuata zitakuwa kubwa zaidi iwapo hilo litatokea.

    Mkuu wa majeshi ya Iran, Meja Jenerali Mohammad Bagheri, aliiambia TV ya serikali kwamba ikiwa Israel italipiza kisasi, jibu la Iran litakuwa "baya zaidi" kuliko shambulio la usiku kucha, Reuters inaripoti.

    Iran pia iliionya Marekani kwamba kuunga mkono kulipiza kisasi kwa Israel kutapelekea kulengwa kwa vituo vya jeshi vya Marekani.

    Awali, ujumbe wa Iran katika Umoja wa Mataifa ulinukuu kifungu cha Mkataba wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kujilinda, chini ya Kifungu cha 51, na kusema kuwa nchi hiyo ilizingatia "suala hili... na kuhitimisha" baada ya mashambulizi yake dhidi ya Israel, huku pia ikiionya Israel dhidi ya kufanya "kosa lingine".

    Soma zaidi:

  14. 'Bado haijaisha': Waziri wa Ulinzi wa Israel

    .

    Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant amesema amekamilisha tathmini ya shughuli zinavyoendeshwa vitani na maafisa wakuu katika taasisi ya ulinzi ya Israel.

    "Pamoja na Marekani na washirika wengine, tuliweza kulinda eneo la Jimbo la Israel. Uharibifu mdogo sana ulisababishwa - hii ni matokeo ya shughuli za kuvutia za IDF," alisema.

    Hata hivyo, aliongeza: "Kampeni bado haijaisha - lazima tuwe macho na makini kwa maagizo yaliyochapishwa na IDF na Kamandi ya Nyumbani. Lazima tujitayarishe kwa kila hali. Baada ya kusema haya, tumezuia wimbi kubwa zaidi [la mashambulizi], na tulifanya hivyo kwa mafanikio.”

  15. 'Tutashinda': Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu

    .

    Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema nchi yake "itashinda", vita katika ujumbe wake kwenye mtandao wa Twitter.

    Awali, alihutubia nchi, akisema jeshi liko "tayari kwa hali yoyote", baada ya Iran kuanzisha mashambulizi ya ndege zisizo na rubani na makombora usiku kucha.

    Soma zaidi:

  16. Israel yadungua ndege 300 za Iran zisizo na rubani na makombora kwa usaidizi wa Marekani - IDF

    .

    Iran imerusha zaidi ya ndege zisizo na rubani 300 na makombora dhidi ya Israeli - asilimia 99 ya ndege hizo zilidunguliwa, jeshi la Israeli limesema.

    Katika taarifa kwa televisheni, msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Israel Daniel Hagari pia alisema kuwa baadhi ya milipuko ya usiku ilitoka Iraq na Yemen.

    Ving'ora vilisikika kwenye anga za Yerusalemu

    Ishara ya kwanza ya shambulio hilo ilikuwa karibu jioni wakati jeshi la Israei lilipotangaza vikosi vyake viko macho na kwamba makumi ya ndege za kivita zilikuwa angani.

    Mamlaka ilisema mikusanyiko ya watu wengi na shughuli za elimu zilipaswa kusitishwa. Na kisha msemaji wa jeshi alithibitisha hilo: Ndege zisizo na rubani za Iran zilikuwa zimerushwa na zilikuwa zikielekea Israel.

    Muda mfupi baadaye, ilionekana wazi kuwa vikosi vya washirika walikuwa wakisaidia kuzuia ndege zisizo na rubani na makombora kabla ya kufika Israel.

    Soma zaidi:

  17. Hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja ikiwa ni tarehe 14/04/2024