Sudan: Faru dume wa kipekee aliyekuwa amesalia duniani afa

Huyu ni faru pekee wa kiume aina ya 'Northern Whire Rhino' aliyesalia ulimwenguni

Sudan, faru pekee wa kiume aina ya Northern White Rhino (Faru Weupe wa Kaskazini) aliyekuwa amesalia hai duniani, amekufa akiwa na miaka 45, shirika la Ol Pejeta limetangaza.

Faru huyo alikuwa akitibiwa kwa muda na matabibu katika shamba kubwa la uhifadhi wa wanyama la kituo hicho kwa muda kutokana na matatizo yaliyotokana na kuzeeka kwake.

Alikuwa na vidonda ambavyo vilikuwa vinakosa kupona kutokana na umri wake.

Shirika la Ol Pejeta limesema hali yake ilidhoofika sana katika kipindi cha saa 24 zilizopita.

"Hakuweza hata kusimama na alikuwa anateseka sana," Ol Pejeta wamesema kupitia taarifa.

"Matabibu wa wanyama kutoka kituo cha uhifadhi wa wanyama cha Dvur Kralove kutoka Jamhuri ya Czech, Ol Pejeta na Shirika la Wanyamapori kenya waliamua kukatisha uhai wake."

Sudan alikuwa maarufu sana duniani na alikuwa nembo ya kutetea juhudi za kupigana na ujangili na kuwaokoa wanyama walio katika hatari ya kuangamia.

Sudan the white rhino

Alinusurika kuuawa porini alipohamishiwa katika kituo cha kuhifadhi wanyama cha Dvur Kralove nchini Jamhuri ya Czech miaka ya 1970.

Mwaka 2009, alirejeshwa Afrika na kuanza kutunzwa katika kituo cha Ol Pejeta katika jimbo la Laikipia.

Alichangia kuendeleza faru wa aina yake kwa kutungisha mimba faru wengine na kuchangia kuzaliwa kwa faru wengine wawili wa aina yake ambao sasa ndio pekee waliosalia hai.

Ruka Twitter ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Mwisho wa Twitter ujumbe, 1

Faru hao kwa jina Najin na Fatu ni wa kike lakini ni tasa.

"Kadhalika, chembe za jeni zake zilichukuliwa na kuhifadhiwa jana kabla ya kifo chake kwa matumaini kwamba zitasaidia katika juhudi za siku za usoni za kuwazalisha faru kupitia teknolojia ya jeni na seli," Ol Pejeta wamesema.

Ruka Twitter ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Mwisho wa Twitter ujumbe, 2

Matumaini pekee sasa ya kuendeleza faru wa aina ya Northern White Rhino ni kupitia teknolojia ya kutungisha mbegu kwenye mayai ya mnyama nje ya mwili wa mnyama huyo, maarufu kama IVF.

Sudan the white rhino

Chanzo cha picha, Getty

Hilo linatarajiwa kufanyika kwa kutumia mayai yaliyovunwa kutoka kwa faru jike walio hai kwa sasa pamoja na mbegu za kiume kutoka kwa faru wengine wa kaskazini.

Shughuli ya kutungisha mbegu mayai hayo ikifanikiwa, basi faru wa karibu aina ya Southern White Rhino watatumiwa kubeba mimba hiyo.

Kutumiwa kwa mtandao wa Tinder

Mwaka uliopita, shirika la Ol Pejeta lilizindua kampeni ya kuchangisha pesa kupitia kufungua akaunti kwenye mtandao wa kutafuta wapenzi wa Tinder.

Lengo lilikuwa kuchangisha dola milioni 9 zitakazofadhili utafiti wa kutafuta mbinu mbadala za kutumia mbegu zao kuzalisha.

Tinder inaongoza ulimwenguni miongoni mwa mitandao ya kijamii inayotumika kutafuta marafiki na wapenzi.

Ruka Twitter ujumbe, 3
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Mwisho wa Twitter ujumbe, 3

Kupitia kampeni #TheMostEligibleBachelor, Tinder walitumai picha ya Sudan ingeonekana katika mataifa 190 ulimwenguni.

Kampeni hiyo ilidhaniwa kuwa njia pekee iliyosalia ya kuokoa faru hao wanaokabiliwa na hatari kubwa ya kuangamia.